Header Ads

test

HABARI KAMILI KUHUSU KIFO CHA SHAROMILLIONEA

Mwaka mmoja haujaisha, bado mioyo ya watanzania wapenda burudani ikiwa bado njia panda ikitafakali yaliyokwisha kutokea, kukutwa na matukio magumu ya kihistoria kuikumba sanaa ta Tanzania.

Nasikitika kusema Sharo Milione hatunae kwasasa, baada ya kupata ajali ya gari mkoani Tanga wakati akitokea Dar es salaam akiwa mwenyewe ndani ya gari. Kamanda wa polisi wa mkoa wa Tanga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na mwili wa marehemu uko mochwali mkoani Tanga.

Ushuda wa Majonzi: Mara ya mwisho Anna Peter wa East Africa Radio Alhamis iliyopita alifanya nae mahojiano na hivi ndivyo alivyoeleza jinsi alivyoghubikwa na majonzi.....


"Wiki hata haijapita alifanya Interview yake ya kwanza na ya mwisho East Africa Radio, kama ulisikiliza utakumbuka nilimtania marehemu Sharomilionea kuwa mimi na yeye tuna historia yetu ambayo watu wengi hawajui....
Tulifanya nae movie ya 'Kimela' mwaka 2006 na yeye alikuwa anashika boom mic ana akawa anapenda kuwa karibu na mimi coz alikua anajua mimi mtangazaji(kipindi hicho Times Fm).
 Alikuwa akinambia Dada Anna mimi napenda kuimba,napenda kutangaza na iko siku nitatoka.
Tangu mwaka 2006 kwa mara ya kwanza Alhamisi tarehe 22 ndo nilifanya nae interview ya kwanza na yeye tho alishanipigia simu kama mara 2 akitaka interview na akinikumbusha kuwa tuliwahi kuonana, but mimi nikawa sina kumbukumbu mpaka tulipokuja kuonana Ana kwa ana.
Tulivyoanana Akanikumbusha kuwa Dada Anna uliwahi kusema utanisaidia, na kweli umethibitisha maneno yakoo.....Nataka kujaribu kukumbuka tulivyozungumza kwenye ile interview but siwezii ....#RIP kweli kifo hakichagui mtu......Poleni ndugu jamaa na marafiki pia".
ITIZAME PICHA YAGARI ALIYOPATA NAYO AJALI

YANAYOJIRI KWENYE MSIBA WA SHARO MILLIONEA:

Hali ya mzee King Majuto presha imepanda na hali kuzidi kuwa mbaya kutokana na kupata taarifa za msiba wa Sharo Milionea.

Mjomba wa marehemu Sharo Millionea, Bwana Omary Fundikira asema marehemu anatarajiwa kuzikwa siku ya kesho, Jumatano. Hii ni kutokana na msanii mwenzake John Maganga kuzikwa leo.

Mkuu wa polisi mkoa wa Tanga RPC Costantine Massawe asema Hussein Ramadhani (Sharo Milionea) alikuwa mwenyewe katika gari na ilipotokea ajali gari lilimrusha nje na kufariki hapohapo.

Pia rafiki wa marehemu bwana Mohamed Ismail ambaye ndiye aliyemuazimisha gari alilopata nalo ajali, asema ilitakiwa waongozane kwenda Tanga pamoja ila alishindwa maana alipata majukumu mengine.
 
HII NDIYO MESEJI YAKE YA MWISHO KWENYE BBM

HII NDIYO PICHA YAMWISHO ALIYOPIGWA BAADA YA AJALI HIYO

msikilize kamanda wa polisi akizungumzia ajali hiyo